![](https://i2.wp.com/zanzibar24.co.tz/wp-content/uploads/kanisa.jpg?resize=800%2C445)
Wananchi wenye hasira kali wamevamia katika eneo la Kanyogoga Wilaya ya Gulu nchini Uganda na kuchoma Kanisa moja muda mfupi baada ya ibada ya asubuhi, kwa madai kuwa linawaletea pepo wachafu.
Wakaazi wa eneo hilo lililoko Kaskazini mwa nchi hiyo wameeleza kuwa wamekuwa wakichukizwa na mienendo ya ibada ya Kanisa hilo linalofahamika kama ‘Jesus is the Living Stone’ ambayo ni kinyume cha mafundisho ya Kikristo.
Jeshi la Polisi limethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kueleza kuwa Kanisa hilo lilikuwa limefungwa na Serikali lakini mchungaji wake alikaidi amri hiyo halali.
No comments:
Post a Comment