Thursday, 17 January 2019

Wanaofanya ulanguzi wa tiketi wapewa onyo

Akizungumza  kwenye  maonesho ya tano ya  biashara  Maisara Kepteni  Ramadhan  Shehe  kutoka kwenye  shirika hilo  amesema shirika linapokea kesi za upandishwa wa bei za tiketi  kiholela  kwa abiria wanaosafiri kwenda Dar es salamu na Pemba  kitendo ambavyo  linaondoa nguvu kazi ya shirika hilo.
Amesema tayari hatua za kisheria zinaendelea kuchukuliwa kwa wanaobainika  kupandisha  bei kubwa  za tiketi  kwa abiria kwani hali hiyo itakapoachiwa  itawaumiza wanancha hasa wenye vipato vya chini.
Aidha amesema  bei zote za tiketi  zilizowekwa kisheria zinatambulika kwa  daraja la chini ambayo ni economcy  ni elfu 25,kwa daraja la kati ni elfu35 na kwa VIP ni elfu 50 kwa boti za kampuni ya azam na kwa shirika la meli zanzibar bei zake kwa daraja la chini ni shilling elfu 18.
Hata hivyo amesema umewekwa ulinzi wa kutosha kwa  hivyo abiria yoyote atakaeuziwa bei kubwa ya tiketi ametakiwa kutoa taarifa kwa shirika au askari wa karibu.
Akizungumzia suala  zima la kuimarika kwa huduma za usafirishaji amesema shirika limepiga hatua kwani wanayo meli ya mapinduzi 2 ambayo kwa sasa inafanya kazi vizuri  na  kwa meli ya maendeleo ipo njiani kufanyiwa matengenezo  ili kuweza kutoa huduma za usafirishaji lakini pia wanampango wa kuleta meli nyengine mpya ya abiria kwa mwaka huu.

No comments:

Post a Comment